Breacking

https://jerome24news.blogspot.com/

Monday, May 28, 2018

Sheria ya kikomo cha umri wa kugombea urais yaidhinishwa na mahakama Uganda

 Sheria ya kikomo cha umri wa kugombea urais yaidhinishwa na mahakama Uganda

Mahakama ya katiba nchini Uganda imeidhinisha mageuzi ya katiba yaliondoa kikomo kwa umri wa kugombea urais.
Majaji wanne kati ya watano wa jopo la majaji wamesema mageuzi hayo hayakiuki katiba, na pia hayendi kinyume na hsri aya muongozo wa bunge nchini.
Awali umri wa mwisho kwa kugombea ilikuwa miaka 75.
Hii ina maana Rais wa nchi hiyo Yoweri Kaguta Museveni atakua huru kugombea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021.
Kikao cha kutoa uamuzi huo uliowasilishwa katika mahakama kuu huko Mbale kilianza kwa naibu jaji mkuu, Alfonse Owiny-Dollo, kuanza kwa kuomba radhi kwa mahakama kuchelewa kuanza kwa muda uliopangwa awali.

No comments:

Post a Comment